Pages

Labels

Monday, November 17, 2014

WAANDAMANA KUPINGA VITENDO VYA WANAWAKE KUVULIWA NGUO:KENYA


Ikiwa tamaduni za muafrika zinawataka watu wavae nguo za staha na heshima, huko Kenya wanawake na baadhi ya wanaume wameandamana wakishinikiza kuwa wanawake wanauhuru wakuvalia mavazi wanayofurahishwa nayo.

Hatua hiyo imekuja baada ya mwanamke mmoja kuvuliwa nguo na wanaume wiki iliyopita kwenye kituo cha magari cha abiria huko Nairobi kisa amevaa nguo fupi. Waandamani wamepinga vikali kitendo hicho.

Baadhi ya wanaharakati, wasanii na watu maarufu wamesema kwa hali hiyo basi hata wanaume wanaovalia mlegezo nao wavuliwe nguo.
Maandamano hayo yalienda sambamba na kauli mbiu ya "ma dress my choice"
Chanzo: BBC

0 comments:

Post a Comment