Pages

Labels

Tuesday, September 2, 2014

KENYA KUWANASA WAFANYA KAZI BANDIA.



Serikali ya Kenya imezindua mfumo wa kielektroniki utakao iwezesha kugundua wafanyakazi bandia wa utimishi wa umma.

Akizindua shughuli za kung’amua wafanyakazi bandia jana raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema lengo sio kuwafukuzisha kazi wafanyakazi wa umma bali nikuhakikisha wakenya wanapata huduma bora wanazo hitaji.

Shughuli hizo zina husisha mfumo wa kuchukua maelezo ya watumishi wote wa umma kupitia njia ya kusajili majina ya wafanyakazi wote kwa njia ya kielektroniki.

Raisi Kenyatta amewataka wafanyakazi wote kushiriki katiza zoezi hilo la usajili ili kukamilisha zoezi hilo kwa muda uliopangwa ili waweze kudhibiti tatizo hilo la wafanyakazi bandia ambalo limekuwa kikwazo kwa serikali.
Chanzo.Irib Swahili

0 comments:

Post a Comment